Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ufunuo 16:17-21

Ufunuo 16:17-21 NENO

Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kubwa ikatoka mle Hekaluni katika kile kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha kuwa!” Kukawa na miali ya radi, ngurumo, radi na tetemeko kubwa la ardhi. Hapajawahi kuwa na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu awepo duniani, kwani lilikuwa tetemeko kubwa ajabu. Ule mji mkubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikaanguka. Mungu akakumbuka Babeli Mkuu na kumpa kikombe kilichojaa mvinyo wa ghadhabu ya hasira yake. Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana. Mvua kubwa ya mawe yenye uzito wa talanta moja ikashuka kutoka mbinguni, ikawaangukia wanadamu. Nao wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya hayo mapigo ya mvua ya mawe, kwa sababu pigo hilo lilikuwa la kutisha.