Zaburi 93
93
Zaburi 93
Mwenyezi Mungu ni mkuu
1Mwenyezi Mungu anatawala, amejivika utukufu;
Mwenyezi Mungu amejivika utukufu
tena amejivika nguvu.
Dunia imewekwa imara,
haitaondoshwa.
2Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani;
wewe umekuwa tangu milele.
3Bahari zimepaza, Ee Mwenyezi Mungu,
bahari zimepaza sauti zake;
bahari zimepaza sauti za mawimbi yake.
4Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu,
ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari:
Mwenyezi Mungu aishiye juu sana ni mkuu.
5Ee Mwenyezi Mungu, sheria zako ni imara;
utakatifu umepamba nyumba yako
pasipo mwisho.
Iliyochaguliwa sasa
Zaburi 93: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.