Zaburi 34:4-7
Zaburi 34:4-7 NEN
Nilimtafuta BWANA naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote. Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe. Maskini huyu alimwita BWANA, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote. Malaika wa BWANA hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.