Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 143:1-12

Zaburi 143:1-12 NEN

Ee BWANA, sikia sala yangu, sikiliza kilio changu unihurumie; katika uaminifu na haki yako njoo unisaidie. Usimhukumu mtumishi wako, kwa kuwa hakuna mtu anayeishi aliye mwenye haki mbele zako. Adui hunifuatilia, hunipondaponda chini; hunifanya niishi gizani kama wale waliokufa zamani. Kwa hiyo roho yangu inazimia ndani yangu, moyo wangu ndani yangu unakata tamaa. Nakumbuka siku za zamani; natafakari juu ya kazi zako zote, naangalia juu ya kazi ambazo mikono yako imezifanya. Nanyoosha mikono yangu kwako, nafsi yangu inakuonea kiu kama ardhi kame. Ee BWANA, unijibu haraka, roho yangu inazimia. Usinifiche uso wako, ama sivyo nitafanana na wale washukao shimoni. Asubuhi uniletee neno la upendo wako usiokoma, kwa kuwa nimeweka tumaini langu kwako. Nionyeshe njia nitakayoiendea, kwa kuwa kwako nainua nafsi yangu. Ee BWANA, uniokoe na adui zangu, kwa kuwa nimejificha kwako. Nifundishe kufanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu, Roho wako mwema na aniongoze katika nchi tambarare. Ee BWANA, kwa ajili ya jina lako, hifadhi maisha yangu, kwa haki yako nitoe katika taabu. Kwa upendo wako usiokoma, nyamazisha adui zangu; waangamize watesi wangu wote, kwa kuwa mimi ni mtumishi wako.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 143:1-12

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha