Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mithali 29:9-15

Mithali 29:9-15 NEN

Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani. Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu. Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia. Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu. Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: BWANA hutia nuru macho yao wote wawili. Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote. Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mithali 29:9-15

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha