Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Hesabu 10:29-36

Hesabu 10:29-36 NEN

Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo BWANA amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana BWANA ameahidi mambo mema kwa Israeli.” Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.” Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu. Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na BWANA.” Hivyo waliondoka kutoka mlima wa BWANA, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la BWANA liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika. Wingu la BWANA lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini. Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee BWANA, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.” Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee BWANA, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

Video for Hesabu 10:29-36