Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ayubu 38:1-18

Ayubu 38:1-18 NEN

Kisha BWANA akamjibu Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli. Akasema: “Nani huyu atiaye mashauri yangu giza kwa maneno yasiyo na maarifa? Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza swali, nawe unijibu. “Ulikuwa wapi nilipoweka misingi ya dunia? Niambie, kama unafahamu. Ni nani aliyeweka alama vipimo vyake? Hakika wewe unajua! Ni nani aliyenyoosha kamba ya kupimia juu yake? Je, misingi yake iliwekwa juu ya nini, au ni nani aliyeweka jiwe la pembeni, wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, na malaika wote walipokuwa wakipiga kelele kwa furaha? “Ni nani aliyeifungia bahari milango ilipopasuka kutoka tumbo, nilipoyafanya mawingu kuwa vazi lake, na kuyafungia katika giza nene, nilipoamuru mipaka yake, na kuiweka milango yake na makomeo mahali pake, niliposema, ‘Unaweza kufika mpaka hapa wala si zaidi; hapa ndipo mawimbi yako yenye kiburi yatakapokomea’? “Umepata kuiamrisha asubuhi ipambazuke, au kuyaonyesha mapambazuko mahali pake, yapate kushika miisho ya dunia, na kuwakungʼuta waovu waliomo? Dunia hubadilika kama udongo wa mfinyanzi chini ya lakiri; sura yake hukaa kama ile ya vazi. Waovu huzuiliwa nuru yao, nao mkono wao ulioinuliwa huvunjwa. “Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi? Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti? Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Ayubu 38:1-18