Isaya 12
12
Kushukuru na kusifu
1Katika siku ile utasema:
“Nitakusifu wewe, Ee Mwenyezi Mungu.
Ingawa ulinikasirikia,
hasira yako imegeukia mbali
nawe umenifariji.
2Hakika Mungu ni wokovu wangu;
nitamtumaini wala sitaogopa.
Mwenyezi Mungu, Mwenyezi Mungu,
ni nguvu zangu na wimbo wangu;
amekuwa wokovu wangu.”
3Kwa furaha mtachota maji
kutoka visima vya wokovu.
4Katika siku hiyo mtasema:
“Mshukuruni Mwenyezi Mungu, mliitie jina lake;
julisheni miongoni mwa mataifa yale aliyoyafanya,
tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5Mwimbieni Mwenyezi Mungu, kwa kuwa ametenda mambo makuu,
hili na lijulikane duniani kote.
6Pazeni sauti mwimbe kwa furaha, watu wa Sayuni,
kwa maana mkuu ni yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli miongoni mwenu.”
Iliyochaguliwa sasa
Isaya 12: NENO
Kuonyesha
Shirikisha
Nakili

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia
Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™
Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc.
Imetumiwa kwa ruhusa.
Haki zote zimehifadhiwa duniani kote.
Kiswahili Contemporary Scriptures™
Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc.
Used with permission. All rights reserved worldwide.