Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mwanzo 25:29-34

Mwanzo 25:29-34 NEN

Siku moja Yakobo alipika mchuzi wa dengu, Esau akarudi kutoka porini akiwa na njaa kali. Esau akamwambia Yakobo, “Haraka, nipe huo mchuzi mwekundu! Nina njaa kali sana!” (Hii ndiyo sababu pia aliitwa Edomu.) Yakobo akamjibu, “Niuzie kwanza haki yako ya mzaliwa wa kwanza.” Esau akasema, “Tazama, mimi niko karibu ya kufa, itanifaa nini haki ya mzaliwa wa kwanza?” Yakobo akamwambia, “Niapie kwanza.” Hivyo Esau akamwapia, akamuuzia Yakobo haki yake ya kuzaliwa. Ndipo Yakobo akampa Esau mkate na ule mchuzi wa dengu. Akala na kunywa, kisha akainuka akaenda zake. Kwa hiyo Esau alidharau haki yake ya mzaliwa wa kwanza.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mwanzo 25:29-34