Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mwanzo 25:20-24

Mwanzo 25:20-24 NEN

Isaki alikuwa na umri wa miaka arobaini alipomwoa Rebeka binti Bethueli Mwaramu kutoka Padan-Aramu, nduguye Labani Mwaramu. Isaki akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, kwa sababu alikuwa tasa. BWANA akajibu maombi yake na Rebeka mkewe akapata mimba. Watoto wakashindana tumboni mwake, akasema, “Kwa nini haya yanatokea kwangu?” Kwa hiyo akaenda kumuuliza BWANA. BWANA akamjibu, “Mataifa mawili yamo tumboni mwako, na mataifa hayo mawili kutoka ndani yako watatenganishwa. Mmoja atakuwa na nguvu zaidi kuliko mwingine, na yule mkubwa atamtumikia yule mdogo.” Wakati wake wa kujifungua ulipotimia, walikuwepo mapacha wa kiume tumboni mwake.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Mwanzo 25:20-24