Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 36:1-7

Kutoka 36:1-7 NEN

Kwa hiyo Bezaleli, Oholiabu na kila mtu BWANA aliyempa ustadi na uwezo wa kujua jinsi ya kufanya kazi zote za kujenga mahali patakatifu wataifanya hiyo kazi kama vile BWANA alivyoagiza.” Ndipo Mose akawaita Bezaleli na Oholiabu na kila mtu mwenye ustadi ambaye BWANA alikuwa amempa uwezo na mwenye kupenda kuja na kufanya kazi. Wakapokea kutoka kwa Mose sadaka zote ambazo Waisraeli walikuwa wameleta ili kuifanya kazi ya ujenzi wa Mahali Patakatifu. Nao watu wakaendelea kuleta sadaka za hiari kila asubuhi. Ikafika wakati mafundi wote wenye ujuzi waliokuwa wakiifanya kazi yote ya mahali patakatifu wakasimamisha kazi zao, wakaja na kumwambia Mose, “Watu wanaleta vitu vingi kuliko tunavyohitaji kwa ajili ya kazi hii ambayo BWANA ameagiza ifanyike.” Ndipo Mose akatoa agizo, nao wakapeleka neno hili katika kambi yote: “Mtu yeyote mwanaume au mwanamke asilete tena kitu chochote kwa ajili ya sadaka ya mahali patakatifu.” Hivyo watu wakazuiliwa kuleta zaidi, kwa sababu walivyokuwa navyo tayari vilitosha na kuzidi kuifanya kazi yote.