Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Kutoka 34:27-35

Kutoka 34:27-35 NEN

Kisha BWANA akamwambia Mose, “Andika maneno haya, kwa maana kulingana na maneno haya, nimefanya Agano na wewe pamoja na Israeli.” Mose alikuwa huko pamoja na BWANA kwa siku arobaini usiku na mchana bila kula chakula wala kunywa maji. Naye akaandika juu ya vibao maneno ya Agano, yaani zile Amri Kumi. Mose alipoteremka kutoka Mlima Sinai akiwa na vile vibao viwili vya Ushuhuda mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa ukingʼaa, kwa sababu alikuwa amezungumza na BWANA. Aroni na Waisraeli wote walipomwona Mose, kuwa uso wake unangʼaa, waliogopa kumkaribia. Lakini Mose akawaita, kwa hiyo Aroni na viongozi wote wa jumuiya wakarudi, naye akazungumza nao. Baadaye Waisraeli wote wakamkaribia, naye akawapa amri zote BWANA alizompa katika Mlima wa Sinai. Mose alipomaliza kuzungumza nao, akaweka utaji kwenye uso wake. Lakini kila wakati Mose alipoingia mbele za BWANA kuzungumza naye, aliondoa ule utaji mpaka alipotoka nje. Naye alipotoka nje na kuwaambia Waisraeli lile ambalo ameagizwa, waliona kuwa uso wake unangʼaa. Kisha Mose angeliweka tena utaji juu ya uso wake mpaka alipokwenda kuzungumza na BWANA.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Kutoka 34:27-35