Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

2 Samweli 22:31-37

2 Samweli 22:31-37 NEN

“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la BWANA halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake. Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya BWANA? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu? Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu. Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu. Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba. Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua. Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na 2 Samweli 22:31-37