Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Samweli 15:17-23

1 Samweli 15:17-23 NEN

Samweli akamwambia, “Ingawa zamani ulijiona mdogo machoni pako mwenyewe, Je, hukuwa kiongozi wa kabila za Israeli? BWANA alikutia mafuta kuwa mfalme juu ya Israeli. Naye akakutuma kwa kazi maalum, akisema, ‘Nenda ukaangamize kabisa wale watu waovu, wale Waamaleki, upigane nao vita mpaka utakapowaangamiza kabisa.’ Kwa nini hukumtii BWANA? Kwa nini ulivamia nyara na kufanya uovu machoni pa BWANA?” Sauli akasema, “Lakini nilimtii BWANA. Nilikamilisha ile kazi ambayo BWANA alinituma. Niliwaangamiza Waamaleki kabisa na kumleta Agagi mfalme wao. Askari walichukua kondoo na ngʼombe kutoka kwenye nyara, zile ambazo ni nzuri sana zimewekwa wakfu kwa Mungu, ili zitolewe dhabihu kwa BWANA Mungu wako huko Gilgali.” Lakini Samweli akajibu: “Je, BWANA anafurahia sadaka za kuteketezwa na dhabihu kama vile kuitii sauti ya BWANA? Kutii ni bora zaidi kuliko dhabihu, nako kusikia ni bora kuliko mafuta ya kondoo dume. Kwa maana kuasi ni kama dhambi ya uaguzi, nao ukaidi ni kama uovu wa kuabudu sanamu. Kwa sababu umelikataa neno la BWANA, naye amekukataa wewe kuendelea kuwa mfalme.”

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha