Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

1 Wafalme 16:29-34

1 Wafalme 16:29-34 NEN

Katika mwaka wa thelathini na nane wa utawala wa Asa mfalme wa Yuda, Ahabu mwana wa Omri akawa mfalme wa Israeli, naye akatawala Israeli akiwa Samaria kwa miaka ishirini na miwili. Ahabu mwana wa Omri akafanya maovu zaidi machoni mwa BWANA kuliko yeyote aliyewatangulia. Kama vile haikutosha kuishi kama Yeroboamu mwana wa Nebati, akamwoa Yezebeli binti wa Ethbaali, mfalme wa Wasidoni, naye akaanza kumtumikia Baali na kumwabudu. Akajenga madhabahu kwa ajili ya Baali katika hekalu la Baali lile alilolijenga huko Samaria. Pia Ahabu akatengeneza nguzo ya Ashera na kufanya mengi ili kumkasirisha BWANA, Mungu wa Israeli, kuliko walivyofanya wafalme wote wa Israeli waliomtangulia. Katika wakati wa Ahabu, Hieli, Mbetheli, akaijenga upya Yeriko. Aliweka misingi yake kwa gharama ya mzaliwa wake wa kwanza Abiramu, na kuweka malango yake kwa gharama ya mwanawe mdogo Segubu, kulingana na neno la BWANA alilosema kupitia Yoshua mwana wa Nuni.

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha