Mataifa walikasirika;
nao wakati wa ghadhabu yako umewadia.
Wakati umewadia wa kuwahukumu waliokufa,
na kuwapa thawabu watumishi wako manabii,
na watakatifu wako pamoja na wale wote
wanaoliheshimu Jina lako,
wakubwa kwa wadogo:
na kuwaangamiza wale wanaoiangamiza dunia.”