1
2 Wathesalonike 2:3
Neno: Maandiko Matakatifu 2024
Mtu yeyote asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja hadi uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.
Linganisha
Chunguza 2 Wathesalonike 2:3
2
2 Wathesalonike 2:13
Lakini inatupasa kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana Isa, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho wa Mungu kwa kuiamini kweli.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:13
3
2 Wathesalonike 2:4
Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:4
4
2 Wathesalonike 2:16-17
Bwana wetu Isa Al-Masihi mwenyewe na Mungu, Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:16-17
5
2 Wathesalonike 2:11
Kwa sababu hii, Mungu anawatumia nguvu ya udanganyifu, ili waamini uongo
Chunguza 2 Wathesalonike 2:11
6
2 Wathesalonike 2:9-10
Kuja kwa yule mwasi kutalingana na vile Shetani hufanya kazi. Atatumia nguvu za aina mbalimbali katika miujiza, na ishara na ajabu za uongo, na katika njia zote ambazo uovu hudanganya wanaoangamia. Wanaangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli ili wapate kuokolewa.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:9-10
7
2 Wathesalonike 2:7
Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo hadi atakapoondolewa.
Chunguza 2 Wathesalonike 2:7
Nyumbani
Bibilia
Mipango
Video