YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 4

4
Kuomba msaada jioni
(Kwa Mwimbishaji: Na ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Daudi)
1Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo.
Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia;
unionee huruma na kusikia sala yangu.
2Jamani, mtaniharibia jina langu mpaka lini?
Mpaka lini mtapenda upuuzi na kusema uongo?
3Jueni kuwa Mwenyezi-Mungu amejiteulia mwaminifu wake.
Mwenyezi-Mungu husikia kila ninapomwomba.
4 # Efe 4:26 Tetemekeni kwa hofu na msitende dhambi;
tafakarini vitandani mwenu na kunyamaza.
5Toeni tambiko zilizo sawa,
na kumtumainia Mwenyezi-Mungu.
6Wengi husema: “Laiti tungepata tena fanaka!
Utuangalie kwa wema, ee Mwenyezi-Mungu!”
7Lakini mimi umenijalia furaha kubwa moyoni,
kuliko ya hao walio na divai na ngano kwa wingi.
8Nalala na kupata usingizi kwa amani;
ee Mwenyezi-Mungu, wewe peke yako waniweka salama.

Currently Selected:

Zaburi 4: BHND

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy