YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 34

34
Sifa kwa wema wa Mungu
(Zaburi ya Daudi alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki)
1Nitamtukuza Mwenyezi-Mungu nyakati zote,
sitaacha kamwe kuzitamka sifa zake.
2Mimi nitaona fahari juu ya Mwenyezi-Mungu,
wanyonge wasikie na kufurahi.
3Mtukuzeni Mwenyezi-Mungu pamoja nami,
sote pamoja tulisifu jina lake.
4Nilimwomba Mwenyezi-Mungu naye akanijibu,
na kuniondoa katika hofu zangu zote.
5Mgeukieni Mungu mpate kufurahi;
nanyi hamtaaibishwa kamwe.
6Maskini alimlilia Mwenyezi-Mungu, naye akamsikia,
na kumwokoa katika taabu zake zote.
7Malaika wa Mwenyezi-Mungu huwalinda wote wamchao,
na kuwaokoa katika hatari.
8 # Taz 1Pet 2:3 Jaribuni mwone Mwenyezi-Mungu alivyo mwema.
Heri mtu anayekimbilia usalama kwake.
9Mcheni Mwenyezi-Mungu enyi watakatifu wake;
maana wenye kumcha hawatindikiwi na kitu.
10Hata wanasimba hutindikiwa na kuona njaa;
lakini wanaomtafuta Mwenyezi-Mungu hawakosi chochote chema.
11Njoni enyi vijana mkanisikilize,
nami nitawafundisha kumcha Mwenyezi-Mungu.
12 # Taz 1Pet 3:10-12 Je, watamani kufurahia maisha,
kuishi maisha marefu na kufurahia mema?
13Basi, acha kusema mabaya,
na kuepa kusema uongo.
14Jiepushe na uovu, utende mema;
utafute amani na kuizingatia.
15Mwenyezi-Mungu huwaangalia waadilifu,
na kusikiliza malalamiko yao;
16lakini huwapinga watu watendao maovu,
awafutilie mbali kutoka duniani.
17Waadilifu wakimlilia Mwenyezi-Mungu yeye huwasikia,
na kuwaokoa katika taabu zao zote.
18Mwenyezi-Mungu yu karibu na waliokufa moyo;
huwaokoa wote waliokata tamaa kabisa.
19Mateso ya mwadilifu ni mengi,
lakini Mwenyezi-Mungu humwokoa kutoka yote.
20 # Taz Yoh 19:36 Huvilinda viungo vya mwili wake wote,
hakuna hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.
21Ubaya huwaletea waovu kifo;
wanaowachukia waadilifu wataadhibiwa.
22Mwenyezi-Mungu huokoa maisha ya watumishi wake,
wote wanaomkimbilia hawataadhibiwa.

Currently Selected:

Zaburi 34: BHN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy