YouVersion Logo
Search Icon

Marko 15

15
Yesu mbele ya Pilato
(Mat 27.1-2,11-14; Lk 23.1-5; Yn 18.28-38)
1Asubui mapema, mara moja wakubwa wa makuhani wakafanya shauri pamoja na wasimamizi wa watu, walimu wa Sheria na wakubwa wote wa baraza. Wakamufunga Yesu, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa Pilato. 2Pilato akamwuliza Yesu: “Wewe ni Mufalme wa Wayuda?”
Yesu akamujibu: “Umesema.”
3Nao wakubwa wa makuhani wakamushitaki Yesu juu ya mambo mengi. 4Basi Pilato akamwuliza tena: “Wewe haujibu hata neno? Angalia mambo haya yote wanayokushitakia!”
5Lakini Yesu hakujibu neno lolote tena, hata Pilato akashangaa.
Yesu anahukumiwa kufa
(Mat 27.15-26; Lk 23.13-25; Yn 18.39–19.16)
6Kila sikukuu ya Pasaka, Pilato alizoea kuwafungulia watu mufungwa mumoja, yule waliyemutaka. 7Kulikuwa mufungwa mumoja, jina lake Baraba, aliyefungwa pamoja na waasi wamoja kwa sababu ya uuaji na uasi walioufanya. 8Watu wakamwendea Pilato, wakaanza kumwomba awatendee kama ilivyokuwa desturi yake. 9Pilato akawajibu, akiwauliza: “Munataka niwafungulie ‘Mufalme wa Wayuda?’ ” 10Alisema vile kwa maana alitambua kwamba wakubwa wa makuhani wamemutoa Yesu kwa sababu walimwonea wivu tu.
11Lakini wakubwa wa makuhani wakawachochea watu wamwombe Pilato awafungulie Baraba. 12Pilato akawauliza watu tena: “Basi munataka nifanye nini na huyu munayemwita Mufalme wa Wayuda?”
13Wakapiga kelele tena wakisema: “Atundikwe juu ya musalaba!”
14Pilato akawauliza: “Alifanya ubaya gani?”
Lakini wakazidi kupiga kelele wakisema: “Atundikwe juu ya musalaba!”
15Kwa kuwa Pilato alitaka kuwapendeza watu, basi akawafungulia Baraba. Na kisha kuamuru wamupige Yesu fimbo, akamutoa kusudi atundikwe juu ya musalaba.
Waaskari wanamuchekelea Yesu
(Mat 27.27-31; Yn 19.2-3)
16Waaskari wakamupeleka Yesu ndani ya upango wa nyumba ya liwali, nao wakaita kundi lao lote wakusanyike. 17Wakamuvalisha Yesu nguo nyekundu, na wakasokota taji na tawi lenye miiba na kumuvalisha nalo juu ya kichwa. 18Kisha wakaanza kumusalimia, wakisema: “Jambo, Mufalme wa Wayuda!” 19Wakamupigapiga tete juu ya kichwa, wakamutemea mate, wakapiga magoti na kuinama mbele yake. 20Walipokwisha kumuchekelea, wakamuvua ile nguo nyekundu na kumuvalisha nguo zake. Kisha wakaondoka naye inje kwa kwenda kumutundika juu ya musalaba.
Yesu anatundikwa juu ya musalaba
(Mat 27.32-44; Lk 23.26-43; Yn 19.17-27)
21Mutu mumoja wa Kurene, aliyeitwa Simoni, baba ya Alesanduro na Rufu, alikuwa akipita katika njia, akitoka kwenye vijiji. Waaskari wakamushurutisha abebe musalaba wa Yesu. 22Wakamufikisha Yesu kwenye pahali palipoitwa Golgota, maana yake “Kilima cha Mufupa wa Kichwa.” 23Wakamupa divai iliyochanganywa na manemane, lakini akaikataa. 24Kisha wakamutundika juu ya musalaba, wakagawanyana nguo zake kwa kuzipigia kura, kusudi wajue nguo gani kila mumoja atakazopaswa kutwaa. 25Ilikuwa saa tatu ya asubui wakati walipomutundika juu ya musalaba. 26Na tangazo hili liliandikwa kwa kuonyesha sababu ya kuhukumiwa kwake. “Mufalme wa Wayuda.” 27Vilevile waliwatundika wanyanganyi wawili juu ya misalaba pamoja na Yesu, mumoja kwa upande wake wa kuume na mwingine kwa upande wa kushoto. [ 28Maandiko Matakatifu yanayosema hivi yakatimizwa: “Alihesabiwa pamoja na watenda mabaya.”]
29Watu waliokuwa wakipita pale walimutukana na kutikisatikisa vichwa vyao, wakisema: “Ewe! Wewe uliyetaka kubomoa hekalu na kujenga lingine katika siku tatu, 30ujiokoe sasa mwenyewe, ukijishusha juu ya musalaba!” 31Vilevile wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria kati yao walimusimanga Yesu, wakisemezana: “Aliokoa wengine, lakini sasa anashindwa kwa kujiokoa yeye mwenyewe! 32Kristo, Mufalme wa Waisraeli, ajishushe sasa juu ya musalaba, kusudi nasi tupate kuona na kumwamini.”
Hata wale waliotundikwa pamoja naye walimutukana vilevile.
Kufa kwa Yesu
(Mat 27.45-56; Lk 23.44-49; Yn 19.28-30)
33Ilipokuwa saa sita ya muchana, giza likakuwa katika inchi yote mpaka saa tisa. 34Na saa tisa Yesu akalalamika: “Eloi, Eloi, lama sabaktani” maana yake “Mungu wangu, Mungu wangu, kwa nini umeniacha?”
35Na watu wamoja waliokuwa pale walipomusikia, wakasema: “Musikilize, anamwita Elia.” 36Na mumoja wao akaenda mbio, akachovya kikausho ndani ya divai yenye kuchacha na kukifungia juu ya tete. Kisha akakipandishia Yesu, kusudi apate kunywa, akisema: “Mwache tuone kama Elia atakuja kumushusha juu ya musalaba.”
37Lakini Yesu akalalamika kwa sauti kubwa, akakata roho.
38Basi pazia la hekalu likapasuka vipande viwili toka juu mpaka chini. 39Mukubwa wa waaskari aliyekuwa akisimama mbele ya Yesu, alipoona namna alivyokata roho, akasema: “Hakika mutu huyu alikuwa Mwana wa Mungu!”
40Kulikuwa wanawake wamoja walioangalia kwa mbali. Kati yao kulikuwa Maria wa Magdala, Maria mama ya kijana Yakobo na Yose na mwanamuke mwingine Salome. 41Wanawake hawa ni wale waliomufuata Yesu na kumushugulikia wakati alipokuwa Galilaya. Wanawake wengine wengi waliomufuata mpaka Yerusalema walikuwa pale vilevile.
Kuzikwa kwa Yesu
(Mat 27.57-61; Lk 23.50-56; Yn 19.38-42)
42-43Ilipokwisha kuwa magaribi, Yosefu wa Arimatea, akafika kwa Pilato. (Yosefu alikuwa mutu mwenye heshima katika Baraza Kubwa, na vilevile alikuwa akitazamia kuja kwa Ufalme wa Mungu). Siku ile ilikuwa ya matayarisho ya siku ya Sabato iliyofuata. Kwa hiyo Yosefu akaenda bila woga kwa Pilato kwa kumwomba maiti ya Yesu. 44Pilato akashangaa sana kusikia kwamba Yesu amekwisha kufa. Basi akamwita yule mukubwa wa waaskari na kumwuliza kama kumepita muda murefu tangia Yesu alipokufa. 45Alipokwisha kuhakikishwa na yule mukubwa wa waaskari kwamba Yesu amekwisha kufa, akamuruhusu Yosefu atwae maiti yake. 46Yosefu akanunua vitambaa, akaondoa maiti ya Yesu juu ya musalaba, akaifungafunga na vile vitambaa na kuiweka ndani ya kaburi lililochimbwa ndani ya jiwe. Kisha wakasukumia jiwe kwenye kiingilio cha lile kaburi. 47Maria wa Magdala na Maria mama ya Yose walikuwa wakiangalia, pahali walipomuzika Yesu.

Currently Selected:

Marko 15: SWC02

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in