YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 50

50
Ibada ya kweli
Zaburi ya Asafu.
1Mungu, Mungu BWANA, amenena, ameiita nchi,
Toka maawio ya jua hadi machweo yake.
2Tokea Sayuni, ukamilifu wa uzuri,
Mungu ameangaza kote.
3Mungu wetu atakuja wala sio kimya kimya,
Moto utakula mbele zake,
na tufani yavuma sana ikimzunguka pande zote.
4 # Mik 6:1,2 Ataziita mbingu zilizo juu,
Na nchi pia, ili awahukumu watu wake.
5 # Isa 13:3; 1 Kor 6:2; 1 The 3:13; Yud 1:14; Kut 24:7; Isa 59:20,21; Ebr 8:6 Nikusanyieni wacha Mungu wangu
Waliofanya agano nami kwa dhabihu.
6Na mbingu zitatangaza haki yake,
Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.
7Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena,
Mimi nitakushuhudia, Israeli;
Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako.
8Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako,
Na kafara zako ziko mbele zangu daima.
9 # Isa 43:23; Mik 6:6; Mdo 17:25 Sitatwaa ng'ombe katika nyumba yako,
Wala beberu katika mazizi yako.
10Maana kila mnyama-pori ni wangu,
Na mifugo juu ya angani elfu.
11Nawajua ndege wote wa milima,
Na wanyama wote wa mashamba ni wangu.
12Kama ningekuwa na njaa singekuambia,
Maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
13Je! Nile nyama ya mafahali!
Au ninywe damu ya mbuzi!
14 # Hes 14:2 Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru;
Mtimizie Aliye Juu nadhiri zako.
15 # Ayu 22:27; Zab 22:23; Mt 5:16; Yn 15:8 Uniite siku ya mateso;
Nitakuokoa, nawe utanitukuza.
16Bali mtu asiye haki, Mungu amwambia,
Una nini wewe kuitangaza sheria yangu,
Na kuliweka agano langu kinywani mwako?
17 # Mit 1:7; 5:12,13; Rum 2:21; 2 The 2:10-12 Maana wewe umechukia maonyo,
Na kuyatupa maneno yangu nyuma yako.
18 # Rum 1:32 Ulipomwona mwizi ulikuwa radhi naye,
Ukashirikiana na wazinzi.
19Umekiachia kinywa chako kinene mabaya,
Na ulimi wako unatunga uongo.
20Umekaa na kumsengenya ndugu yako,
Na mwana wa mama yako umemsingizia.
21 # Mhu 8:11; Rum 2:4 Ndivyo ulivyofanya, nami nikanyamaza;
Ukadhani ya kuwa Mimi ni kama wewe.
Lakini nitakukemea;
Nitakuhukumu kwa hayo yote.
22Yafahamuni hayo,
Ninyi mnaomsahau Mungu,
Nisije nikawararueni,
Asipatikane wa kuwaokoa.
23Atoaye dhabihu za kushukuru,
Ndiye anayenitukuza.
Naye autengenezaye mwenendo wake,
Nitamwonesha wokovu wa Mungu.

Currently Selected:

Zaburi 50: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy