YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 49

49
Upumbavu wa kutegemea mali
Kwa mwimbishaji. Ya Wakorahi. Zaburi.
1Sikieni haya, enyi mataifa yote;
Sikilizeni, ninyi nyote mnaokaa duniani.
2Watu wakuu na watu wadogo wote pia,
Tajiri na maskini wote pamoja.
3Kinywa changu kitanena hekima,
Na fikira za moyo wangu zitakuwa za busara.
4 # Zab 78:2 Nitatega sikio langu nisikie mithali,
Na kufumbua fumbo langu kwa kinubi.
5Kwa nini niogope wakati wa shida,
Ubaya ukinizunguka miguuni pangu?
6Ambao wanazitumainia mali zao,
Na kujisifia wingi wa utajiri wao;
7 # Mt 16:26 Hakuna mtu awezaye kumkomboa ndugu yake,
Wala kumlipa Mungu fidia kwa ajili ya maisha yake,
8 # Ayu 36:18 (Maana fidia ya nafsi zao ina gharama,
Wala hawezi kuitoa hata milele;)
9 # Ebr 9:27; Zab 89:48 ndipo aishi milele asilione kaburi.
10Naam, ataliona, hata wenye hekima hufa;
Mpumbavu na mjinga hupotea pamoja,
Na kuwaachia wengine mali zao.
11Makaburi ni nyumba zao hata milele,
Maskani zao vizazi hata vizazi.
Japo waliwahi kuyamiliki mashamba,
Kwa majina yao wenyewe.
12Lakini mwanadamu hadumu katika heshima,
Bali amefanana na wanyama wapoteao.
13Hiyo ndiyo njia yao, ujinga wao,
Nao walioko baada yao huyaridhia maneno yao.
14 # Dan 7:22; Mal 4:3; Lk 22:30; 1 Kor 6:2; 2 Tim 2:12; Ufu 2:26 Kama kondoo wamewekwa kwenda kuzimu,
Na kifo kitakuwa mchungaji wao;
Watu wanyofu watawamiliki asubuhi;
Miili yao itaoza, kao lao ni kuzimu.
15 # Hos 13:14 Bali Mungu atanikomboa nafsi yangu,
Atanitoa mkononi mwa kuzimu, maana atanipokea.
16Usiogope mtu atakapopata utajiri,
Na fahari ya nyumba yake itakapoongezeka.
17Maana atakapokufa hatachukua chochote;
Utukufu wake hautashuka ukimfuata.
18Ajapojibariki nafsi yake alipokuwa hai,
Na watu watakusifu ukijitendea mema,
19Atakwenda kwenye kizazi cha baba zake
Hawataona nuru hata milele.
20 # Mhu 3:19-21 Mwanadamu mwenye heshima, iwapo hana akili,
Amefanana na wanyama wapoteao.

Currently Selected:

Zaburi 49: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in