YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 142

142
Sala ya ukombozi kutoka kwa watesi
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Ombi.
1 # 1 Sam 22:1; 24:3 Kwa sauti yangu nitamlilia BWANA,
Kwa sauti yangu nitamwomba BWANA dua.
2Nitafunua mbele zake malalamiko yangu,
Shida yangu nitaitangaza mbele zake.
3Roho yangu inapozimia unayajua mapito yangu;
Katika njia niendayo wamenifichia mtego.
4Utazame mkono wangu wa kulia ukaone,
Kwa maana sina mtu anijuaye.
Makimbilio yamenipotea,
Hakuna wa kunitunza roho.
5 # Omb 3:24 BWANA, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu,
Fungu langu katika nchi ya walio hai.
6 # Zab 116:6; 7:1 Ukisikilize kilio changu,
Kwa maana nimedhilika sana.
Uniponye kutoka kwa wanaonifuatia,
Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.
7 # Zab 34:2; 119:17 Uitoe nafsi yangu kifungoni.
Nipate kulishukuru jina lako.
Wenye haki watanizunguka,
Kwa kuwa Wewe unanikirimu.

Currently Selected:

Zaburi 142: SRUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy