YouVersion Logo
Search Icon

Ufu 3

3
Ujumbe wa Sardi
1 # Ufu 5:6; 1:16 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika;
Haya ndiyo anenayo yeye aliye na hizo Roho saba za Mungu, na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, ya kuwa una jina la kuwa hai, nawe umekufa. 2#Eze 34:4Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu. 3#Mt 24:43-44; Lk 12:39-40; Ufu 16:15; 1 The 5:2Basi kumbuka jinsi ulivyopokea, na jinsi ulivyosikia; yashike hayo na kutubu. Walakini usipokesha, nitakuja kama mwivi, wala hutaijua saa nitakayokuja kwako. 4#Yud 1:23Lakini unayo majina machache katika Sardi, watu wasioyatia mavazi yao uchafu. Nao watakwenda pamoja nami hali wamevaa mavazi meupe, kwa kuwa wamestahili. 5#Kut 32:32-33; Zab 69:28; Ufu 4:4; 6:11; 7:9; 20:12; Flp 4:3; Mt 10:32; Lk 12:8Yeye ashindaye atavikwa hivyo mavazi meupe, wala sitalifuta kamwe jina lake katika kitabu cha uzima, nami nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu, na mbele ya malaika zake. 6Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
Ujumbe kwa Filadelfia
7 # Isa 22:22; Ayu 12:14 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika;
Haya ndiyo anenayo yeye aliye mtakatifu, aliye wa kweli, aliye na ufunguo wa Daudi, yeye mwenye kufungua wala hapana afungaye, naye afunga wala hapana afunguaye. 8#1 Kor 16:9Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu. 9#Isa 49:23; 60:14; 43:4; 45:14; 66:23Tazama, nakupa walio wa sinagogi la Shetani, wasemao kwamba ni Wayahudi, nao sio, bali wasema uongo. Tazama, nitawafanya waje kusujudu mbele ya miguu yako, na kujua ya kuwa nimekupenda. 10#Ufu 13:10; Ebr 10:36; Lk 21:19; 2 Tim 2:12Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi. 11#Ufu 1:3; 2:5,10Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako. 12#Ufu 21:2; 14:1; 22:4; Eze 48:35; Gal 2:9; Isa 62:2; 65:15Yeye ashindaye, nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo tena kabisa, nami nitaandika juu yake jina la Mungu wangu, na jina la mji wa Mungu wangu, huo Yerusalemu mpya, ushukao kutoka mbinguni kwa Mungu wangu, na jina langu mwenyewe, lile jipya. 13Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.
Ujumbe kwa Laodikia
14 # Mit 8:22; Zab 89:37; Yn 1:3; Kol 1:15 Na kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika;
Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina, Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli, mwanzo wa kuumba kwa Mungu. 15#Ufu 2:2; Rum 12:11Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. 16Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu. 17#Hes 12:8; 1 Kor 3:18; 4:8Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi. 18#1 Pet 1:7; Isa 55:1; Ufu 16:15Nakupa shauri, ununue kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, upate kuwa tajiri, na mavazi meupe upate kuvaa, aibu ya uchi wako isionekane, na dawa ya macho ya kujipaka macho yako, upate kuona. 19#Mit 3:12; Ebr 12:6; 1 Kor 11:32Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu. 20#Mk 13:14; Yn 14:23; Lk 12:36; 22:29Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. 21#Mt 19:28Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi. 22Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa.

Currently Selected:

Ufu 3: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in