1
Ufu 3:20
Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia
Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.
Compare
Explore Ufu 3:20
2
Ufu 3:15-16
Nayajua matendo yako, ya kuwa hu baridi wala hu moto; ingekuwa heri kama ungekuwa baridi au moto. Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
Explore Ufu 3:15-16
3
Ufu 3:19
Wote niwapendao mimi nawakemea, na kuwarudi; basi uwe na bidii, ukatubu.
Explore Ufu 3:19
4
Ufu 3:8
Nayajua matendo yako. Tazama, nimekupa mlango uliofunguliwa mbele yako, ambao hapana awezaye kuufunga, kwa kuwa unazo nguvu kidogo, nawe umelitunza neno langu, wala hukulikana jina langu.
Explore Ufu 3:8
5
Ufu 3:21
Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi, kama mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba yangu katika kiti chake cha enzi.
Explore Ufu 3:21
6
Ufu 3:17
Kwa kuwa wasema, Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu; nawe hujui ya kuwa wewe u mnyonge, na mwenye mashaka, na maskini, na kipofu, na uchi.
Explore Ufu 3:17
7
Ufu 3:10
Kwa kuwa umelishika neno la subira yangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kuharibiwa iliyo tayari kuujilia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya nchi.
Explore Ufu 3:10
8
Ufu 3:11
Naja upesi. Shika sana ulicho nacho, asije mtu akaitwaa taji yako.
Explore Ufu 3:11
9
Ufu 3:2
Uwe mwenye kukesha, ukayaimarishe mambo yaliyosalia, yanayotaka kufa. Maana sikuona matendo yako kuwa yametimilika mbele za Mungu wangu.
Explore Ufu 3:2
Home
Bible
Plans
Videos