YouVersion Logo
Search Icon

Zab 114

114
Maajabu ya Mungu Wakati wa kutoka Misri
1 # Kut 12:51 Haleluya.
Israeli alipotoka Misri,
Na Yakobo katika watu wa lugha ya kigeni.
2Yuda ilikuwa patakatifu pake,
Israeli milki yake.
3 # Kut 14:21; Yos 3:16 Bahari iliona ikakimbia,
Yordani ilirudishwa nyuma.
4 # Zab 29:6; 68:16; Hab 3:6 Milima iliruka kama kondoo waume,
Vilima kama wana-kondoo.
5Ee bahari, una nini, ukimbie?
Yordani, urudi nyuma?
6Enyi milima, mruke kama kondoo waume?
Enyi vilima, kama wana-kondoo?
7Tetemeka, Ee nchi, mbele za uso wa Bwana,
Mbele za uso wa Mungu wa Yakobo.
8 # Kut 17:1-7; Hes 20:2-13; Zab 107:35 Augeuza mwamba kuwa ziwa la maji,
Jiwe gumu kuwa chemchemi.

Currently Selected:

Zab 114: SUV

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in

YouVersion uses cookies to personalize your experience. By using our website, you accept our use of cookies as described in our Privacy Policy