YouVersion Logo
Search Icon

Zaburi 13

13
Zaburi 13
Sala Ya Kuomba Msaada
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Mpaka lini, Ee Bwana? Je, utanisahau milele?
Utanificha uso wako mpaka lini?
2 Nitapambana na mawazo yangu mpaka lini,
na kila siku kuwa na majonzi moyoni mwangu?
Adui zangu watanishinda mpaka lini?
3 Nitazame, unijibu, Ee Bwana Mungu wangu.
Yatie nuru macho yangu,
ama sivyo nitalala usingizi wa mauti.
4 Adui yangu atasema, “Nimemshinda,”
nao adui zangu watashangilia nitakapoanguka.
5 Lakini ninategemea upendo wako usiokoma;
moyo wangu unashangilia katika wokovu wako.
6 Nitamwimbia Bwana,
kwa kuwa amekuwa mwema kwangu.

Currently Selected:

Zaburi 13: NEN

Highlight

Share

Copy

None

Want to have your highlights saved across all your devices? Sign up or sign in