YouVersion 標識
搜索圖示

Mwanzo UTANGULIZI

UTANGULIZI
Kitabu cha Mwanzo ndicho cha kwanza katika orodha ya vitabu vya Biblia. Jina Mwanzo linatokana na kitabu chenyewe (1:1) kwa maana ya asili na chanzo cha ulimwengu, mtu, dhambi, kifo na taifa la Israeli. Jambo la msingi ni Mungu na mtu katika uhusiano wao na pia mpango wa Mungu wa wokovu na uteule wa watu wa wake.
Mungu ndiye Muumba wa vitu vyote. Mungu alimwumba mtu, lakini mtu huyo alimwasi Muumba wake, na kwa uasi wake watu wote wakawa wenye dhambi. Matokeo ya dhambi yakawa kifo. Kwa kuwa tangu mwanzo Mungu aliahidi kuujalia uumbaji wake baraka zake. Ndipo hata mtu alipoasi, Mungu aliendelea kujifunua kwake, kunena na wateule wake, kuwapa wajibu na kuwabariki.
Yaliyomo:
1. Simulizi la awali kuhusu ulimwengu na mtu, Sura 1—11
(a) Kuumba ulimwengu (1—2)
(b) Uasi na kuanguka kwa mtu (3)
(c) Uasi unaongezeka (4—5)
(c) Nuhu na gharika (6—9)
(d) Mnara wa Babeli (10—11)
2. Historia ya awali ya Waisraeli, Sura 12—50
(a) Habari za Abrahamu na watoto wake (12—24)
(b) Habari za Yakobo (25—36)
(c) Habari za Yusufu (37—50)

醒目顯示

分享

複製

None

想要在所有設備上保存你的醒目顯示嗎? 註冊或登入

YouVersion 使用 cookie 來個性化你的體驗。透過使用我們的網站,你即接受我們按照我們的 隱私政策所述來使用 cookie。