SOMA BIBLIA KILA SIKU 01/20Mfano

Yesu alizaliwa kuwa Mfalme wa Wayahudi, wakati Mfalme Herode alipotawala. Soma pia Yn 18:36-37 kuelewa ufalme wa Yesu ulivyo. “Mamajusi” maana yake ni “wenye hekima”. Walifika Yerusalemu wakiongozwa na nyota. Walimwuliza Mfalme Herode, Yuko wapi Mfalme wa Wayahudi aliyezaliwa? Herode alifadhaika sana na maelezo yao. Alifikiri atanyang’anywa ufalme, akaanza kuhangaika akiita watu maarufu ili kuwauliza, Kristo azaliwa wapi?"Kristo", maana yake ni "mpakwa mafuta wa Bwana". Yaani Yesu ni Mfalme aliyepewa kutimiza unabii wa Isaya 9:6-7 unaosema, Kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani. Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 01/20 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu hasa katika kitabu cha Mathayo, Kutoka, Zaburi na Isaya. Mpango huu una maelezo mafupi yatakayokusaidia kuelewa zaidi Neno la Mungu. Anza mwaka wa 2020 kwa kujifunza Neno la Mungu kupitia mpango huu.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku Julai 2021

Upendo Wa Bure

Soma Biblia Kila Siku Februari 2021

Soma Biblia Kila Siku Mei 2021

Roho Mtakatifu - Tuna Uwezo Wa Kuwaka Moto Au La?

Soma Biblia Kila Siku 11/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Januari 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021
