Soma Biblia Kila Siku 8Mfano

Paulo alijieleza kwa Wayahudi kuhusu sababu ya yeye kuwepo huko. Alifikiri huenda wameisikia habari yake na kutaka kumwua. Lakini walikuwa hawajasikia lolote, na walikuwa tayari kumsikiliza (m.21-22: Wakamwambia, Sisi hatukupata nyaraka zenye habari zako kutoka Uyahudi, wala hapana ndugu hata mmoja aliyefika hapa na kutupasha habari, au kunena neno baya juu yako.
Lakini tunataka kusikia kwako uonavyo wewe; kwa maana katika habari za madhehebu hiyo imejulikana kwetu kwamba inanenwa vibaya kila mahali). Hatusikii zaidi kuhusu kesi yake Paulo. Ila tunaona kwamba kwa miaka miwili hii alipokaa Rumi alikuwa na uhuru kiasi kikubwa. Muda wote alitumia kwa ajili ya kufundisha watu neno la Mungu (m.30-31:Akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea, akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu). Baadaye alifunguliwa (tunavyojua ilitokea mwaka 62 BK) na kufanya tena safari ya misioni. Mwisho akauawa na Kaisari Nero huko Rumi mwaka 64 BK.
Andiko
Kuhusu Mpango huu

Soma Biblia Kila Siku 8 ni mpango mzuri wa kusoma Biblia sehemu kwa sehemu kila siku hasa katika kitabu cha Matendo ya Mitume, Kumbukumbu la Torati, na Yohana pamoja na maelezo yatakayokusaidia kutafakari na kuelewa Neno la Mungu kwa urahisi.
More
Tunapenda kumshukuru Soma Biblia kwa kutoa mpango huu. Kwa habari zaidi, tafadhali tembelea: http://www.somabiblia.or.tz
Mipangilio yanayo husiana

Soma Biblia Kila Siku 12

Soma Biblia Kila Siku 9

MWANGA Kuvutiwa Maishani Na Mwanga Ajabu Wa Mungu

Soma Biblia Kila Siku 06/2020

BibleProject | Safari ya Kujifunza Kutoka Luka Na Matendo

Soma Biblia Kila Siku Aprili 2021

Soma Biblia Kila Siku Machi 2021

Soma Biblia Kila Siku 10

Soma Biblia Kila Siku 11
