Zaburi 44:20-26
Zaburi 44:20-26 Biblia Habari Njema (BHN)
Tungalikuwa tumekusahau wewe Mungu wetu, tukamkimbilia mungu wa uongo, ee Mungu, ungalikwisha jua jambo hilo, kwa maana wewe wazijua siri za moyoni. Lakini kwa ajili yako twakikabili kifo kila siku; tunatendewa kama kondoo wanaopelekwa kuchinjwa. Amka, ee Bwana! Mbona umelala? Inuka! Tafadhali usitutupe milele! Mbona wajificha mbali nasi, na kusahau dhiki na mateso yetu? Tumedidimia hata mavumbini, tumegandamana na ardhi. Uinuke, uje kutusaidia! Utukomboe kwa sababu ya fadhili zako.
Zaburi 44:20-26 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu, Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu; Je! Mungu hatalichunguza neno hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo. Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa. Amka, Bwana, mbona umelala? Ondoka, usitutupe kabisa. Mbona unatuficha uso wako, Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu? Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, Tumbo letu limegandamana na nchi. Uondoke, uwe msaada wetu, Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
Zaburi 44:20-26 Neno: Maandiko Matakatifu 2024 (NENO)
Kama tungekuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni, je, si Mungu angegundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo? Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa. Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele. Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu? Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi. Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.
Zaburi 44:20-26 Biblia Habari Njema (BHN)
Tungalikuwa tumekusahau wewe Mungu wetu, tukamkimbilia mungu wa uongo, ee Mungu, ungalikwisha jua jambo hilo, kwa maana wewe wazijua siri za moyoni. Lakini kwa ajili yako twakikabili kifo kila siku; tunatendewa kama kondoo wanaopelekwa kuchinjwa. Amka, ee Bwana! Mbona umelala? Inuka! Tafadhali usitutupe milele! Mbona wajificha mbali nasi, na kusahau dhiki na mateso yetu? Tumedidimia hata mavumbini, tumegandamana na ardhi. Uinuke, uje kutusaidia! Utukomboe kwa sababu ya fadhili zako.
Zaburi 44:20-26 Swahili Revised Union Version (SRUV)
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu, Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu; Je! Mungu hangegundua jambo hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo. Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kama kondoo waendao kuchinjwa. Amka, Bwana, mbona umelala? Ondoka, usitutupe milele. Mbona unatuficha uso wako, Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu? Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, Tumbo letu limegandamana na nchi. Uinuke, uwe msaada wetu, Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
Zaburi 44:20-26 Maandiko Matakatifu ya Mungu Yaitwayo Biblia (SUV)
Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu, Au kumnyoshea mungu mgeni mikono yetu; Je! Mungu hatalichunguza neno hilo? Maana ndiye azijuaye siri za moyo. Hasha! Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; Tunafanywa kondoo waendao kuchinjwa. Amka, Bwana, mbona umelala? Ondoka, usitutupe kabisa. Mbona unatuficha uso wako, Na kusahau kuonewa na kudhulumiwa kwetu? Maana nafsi yetu imeinama mavumbini, Tumbo letu limegandamana na nchi. Uondoke, uwe msaada wetu, Utukomboe kwa ajili ya fadhili zako.
Zaburi 44:20-26 Neno: Maandiko Matakatifu 2024 (NENO)
Kama tungekuwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kunyooshea mikono yetu kwa mungu mgeni, je, si Mungu angegundua hili, kwa kuwa anazijua siri za moyo? Hata hivyo kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa. Amka, Ee Bwana! Kwa nini unalala? Zinduka! Usitukatae milele. Kwa nini unauficha uso wako na kusahau taabu na mateso yetu? Tumeshushwa hadi mavumbini, miili yetu imegandamana na ardhi. Inuka na utusaidie, utukomboe kwa sababu ya upendo wako usio na mwisho.