Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 63

63
Hamu ya kuwa pamoja na Mungu
(Zaburi ya Daudi wakati alipokuwa katika jangwa la Yudea)
1Ee Mungu, wewe u Mungu wangu,
nami nakutafuta kwa moyo;
roho yangu inakutamani kama mtu mwenye kiu;
nina kiu kama nchi kavu isiyo na maji.
2Nimetaka kukuona patakatifuni pako,
niione nguvu yako na utukufu wako.
3Fadhili zako ni bora kuliko maisha,
nami nitakusifu kwa mdomo wangu.
4Nitakushukuru maisha yangu yote;
nitainua mikono yangu na kukuomba.
5Roho yangu inafurahi kama kwa karamu na vinono;
kwa shangwe nitaimba sifa zako.
6Niwapo kitandani ninakukumbuka,
usiku kucha ninakufikiria;
7maana wewe umenisaidia daima.
Kivulini mwa mabawa yako nitashangilia.
8Roho yangu inaambatana nawe kabisa,
mkono wako wa kulia wanitegemeza.
9Lakini hao wanaotaka kuyaangamiza maisha yangu,
watatumbukia chini kwenye makao ya wafu.
10Watauawa kwa upanga,
watakuwa chakula cha mbweha.
11Lakini mfalme atafurahi kwa sababu ya Mungu;
wanaoahidi kwa jina la Mungu watamsifu,
lakini vinywa vya waongo vitafumbwa.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 63: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha