Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 54

54
Sala ya kujikinga na maadui
(Kwa Mwimbishaji: Na ala za nyuzi za muziki. Utenzi wa Daudi wakati mtu mmoja kutoka Zifu alipomwendea Shauli na kumjulisha kuwa Daudi amejificha kwao.)
1Uniokoe, ee Mungu, kwa jina lako;
unitetee kwa nguvu yako.
2Uisikie, ee Mungu, sala yangu;
uyategee sikio maneno ya kinywa changu.
3Watu wenye kiburi wananishambulia;
wakatili wanayawinda maisha yangu,
watu ambao hawamjali Mungu.
4Najua Mungu ni msaada wangu,
Mwenyezi-Mungu hutegemeza maisha yangu.
5Yeye atawaadhibu maadui zangu kwa uovu wao wenyewe;
kwa uaminifu wako, ee Mungu, uwaangamize.
6Nitakutolea tambiko kwa moyo mkunjufu;
nitakushukuru kwa kuwa ni vema.
7Maana umeniokoa katika taabu zangu zote,
nami nimewaona maadui zangu wameshindwa.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 54: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia