Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 53:1-6

Zaburi 53:1-6 BHN

Wapumbavu hujisemea moyoni: “Hakuna Mungu!” Wote wamepotoka kabisa, wametenda mambo ya kuchukiza; hakuna hata mmoja atendaye jema. Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni, aone kama kuna yeyote mwenye busara, kama kuna yeyote anayemtafuta Mungu. Lakini wote wamekosa, wote wamepotoka pamoja, hakuna atendaye mema, hakuna hata mmoja. “Je, hao watendao maovu hawana akili? Wanawatafuna watu wangu kama mikate; wala hawanijali mimi Mungu!” Hapo watashikwa na hofu kubwa, hofu ambayo hawajapata kuiona; maana Mungu ataitawanya mifupa ya adui, hao wataaibika maana Mungu amewakataa. Laiti ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Siyoni! Mungu atakaporekebisha hali ya watu wake, wazawa wa Yakobo watashangilia; Waisraeli watafurahi.

Soma Zaburi 53

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha