Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 16:7-11

Zaburi 16:7-11 BHN

Namsifu Mwenyezi-Mungu kwa kuniongoza, usiku dhamiri yangu yanionya. Namweka Mwenyezi-Mungu mbele yangu daima; yuko pamoja nami, wala sitatikisika. Kwa hiyo nitafurahi kwa moyo wote na kushangilia, nami nitakaa salama salimini. Naam wewe hutaiacha nafsi yangu kuzimu, hutaniacha mimi mwaminifu wako nipate kuoza. Wanionesha njia ya kufikia uhai; kuwako kwako kwanijaza furaha kamili, katika mkono wako wa nguvu mna mema ya milele.

Soma Zaburi 16

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 16:7-11