Toka upeo wa unyonge wangu, nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu. Ee Bwana, sikia sauti yangu, uitegee sikio sauti ya ombi langu. Kama, ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu nani, ee Bwana, angeweza kusalimika? Lakini kwako twapata msamaha, ili sisi tukuheshimu. Namtumainia Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote; nina imani sana na neno lake. Ninamtumainia Mwenyezi-Mungu kuliko walinzi wanavyongojea pambazuko; kuliko walinzi wanavyongojea kuche asubuhi. Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu, maana kwake Mwenyezi-Mungu kuna fadhili, kwake kuna nguvu kubwa ya kutukomboa. Yeye atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika maovu yao yote.
Soma Zaburi 130
Shirikisha
Linganisha Matoleo Yote: Zaburi 130:1-8
Hifadhi mistari, soma bila mtandao, tazama klipu za mafunzo, na zaidi!
YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha
Nyumbani
Biblia
Mipango
Video