Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 130:1-8

Zaburi 130:1-8 BHN

Toka upeo wa unyonge wangu, nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu. Ee Bwana, sikia sauti yangu, uitegee sikio sauti ya ombi langu. Kama, ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu nani, ee Bwana, angeweza kusalimika? Lakini kwako twapata msamaha, ili sisi tukuheshimu. Namtumainia Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote; nina imani sana na neno lake. Ninamtumainia Mwenyezi-Mungu kuliko walinzi wanavyongojea pambazuko; kuliko walinzi wanavyongojea kuche asubuhi. Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu, maana kwake Mwenyezi-Mungu kuna fadhili, kwake kuna nguvu kubwa ya kutukomboa. Yeye atawakomboa watu wa Israeli kutoka katika maovu yao yote.

Soma Zaburi 130

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 130:1-8

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha