Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Obadia 1:15-21

Obadia 1:15-21 BHN

“Siku inakaribia ambapo mimi Mwenyezi-Mungu nitayahukumu mataifa yote. Kama mlivyowatendea wengine, ndivyo mtakavyotendewa, mtalipwa kulingana na matendo yenu. Maana, kama walivyokunywa kikombe cha ghadhabu yangu kwenye mlima wangu mtakatifu ndivyo na mataifa jirani yatakavyokunywa; watakunywa na kupepesuka, wataangamia kana kwamba hawakuwahi kuwapo duniani. “Lakini mlimani Siyoni watakuwapo wale waliosalimika nao utakuwa mlima mtakatifu. Wazawa wa Yakobo wataimiliki tena nchi iliyokuwa yao. Wazawa wa Yakobo watakuwa kama moto na wazawa wa Yosefu kama miali ya moto. Watawaangamiza wazawa wa Esau kama vile moto uteketezavyo mabua makavu, asinusurike hata mmoja wao. Mimi, Mwenyezi-Mungu, nimesema. Wale wanaokaa Negebu wataumiliki mlima Esau; wale wanaokaa Shefela wataimiliki nchi ya Wafilisti. Waisraeli watamiliki nchi za Efraimu na Samaria na watu wa Benyamini wataimiliki nchi ya Gileadi. Waisraeli walio uhamishoni Hala wataimiliki Foinike hadi Sarepta. Watu wa Yerusalemu walio uhamishoni Sefaradi wataimiliki miji ya Negebu. Waokoaji watapanda juu ya mlima Siyoni ili kuutawala mlima Esau; naye Mwenyezi-Mungu atakuwa ndiye Mfalme.”

Soma Obadia 1

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Obadia 1:15-21