Hesabu 6:22-27
Hesabu 6:22-27 BHN
Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Mwambie Aroni na wanawe kwamba hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli: Mtawaambia, ‘Mwenyezi-Mungu awabariki na kuwalinda; Mwenyezi-Mungu awaangalie kwa wema, na kuwafadhili; Mwenyezi-Mungu awaoneshe wema wake na kuwapa amani.’ “Ndivyo watakavyotamka jina langu juu ya Waisraeli, nami nitawabariki.”