Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Mika 2

2
Mika na wapinzani wake
1Ole wao wanaopanga kutenda maovu
wanaolala usiku wakiazimia uovu!
Mara tu kunapopambazuka,
wanayatekeleza kwani wanao uwezo.
2Hutamani mashamba na kuyatwaa;
wakitaka nyumba, wananyakua.
Huwadhulumu wenye nyumba na jamaa zao,
huwanyang'anya watu mali zao.
3Kwa hiyo, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Ninapanga kuwaleteeni nyinyi maafa,
ambayo kamwe hamtaweza kuyakwepa.
Utakuwa wakati mbaya kwenu,
wala hamtaweza kwenda kwa maringo.
4Siku hiyo watu watawasimanga kwa wimbo,
watalia na kuomboleza kwa uchungu, wakisema:
‘Tumeangamia kabisa;
Mwenyezi-Mungu amechukua nchi yetu,
naam, ameiondoa mikononi mwetu.
Mashamba yetu amewagawia waliotuteka.’”#2:4 waliotuteka: Makala ya Kiebrania: Waasi.
5Kwa hiyo hamtagawiwa sehemu yoyote ya ardhi
miongoni mwa watu wake Mwenyezi-Mungu.
Wapinzani wa nabii
6“Usituhubirie sisi.
Mambo kama hayo si ya kuhubiriwa.
Sisi hatutakumbwa na maafa!
7Je, yafaa kusema hivyo, wazawa wa Yakobo?
Je, Mwenyezi-Mungu ameacha uvumilivu wake?
Je, yeye hufanya mambo kama haya?”
Mika
Sivyo! Maneno yangu huwafaa watendao mambo mema.
8Lakini Mwenyezi-Mungu awaambia hivi:
“Nyinyi mnawavamia watu wangu kama adui.
Mnawanyang'anya mavazi yao watu watulivu;
watu wanaopita kwenda zao bila wasiwasi,
na wasio na fikira zozote za vita.
9Mnawafukuza wake za watu wangu
kutoka nyumba zao nzuri;
watoto wao mmewaondolea fahari yangu milele.
10Inukeni mwende zenu!
Hapa hamna tena pa kupumzika!
Kwa utovu wenu wa uaminifu
maangamizi makubwa yanawangojea!
11Kama mtu angetokea akatamka maneno matupu ya uongo
na kusema: ‘Nawatabirieni divai na pombe kwa wingi’,
mhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!
12“Lakini kweli nitawakusanya nyote enyi watu wa Yakobo,
naam, nitawakusanya enyi Waisraeli mliobaki,
niwalete pamoja kama kondoo katika zizi,
kama kundi kubwa la kondoo malishoni;
nanyi mtakuwa kundi la watu wengi.”
13Yule atakayetoboa njia atawatangulia,
nao watalivunja lango la mji na kutoka nje,
watapita na kutoka nje.
Mfalme wao atawatangulia;
Mwenyezi-Mungu mwenyewe atawatangulia.

Iliyochaguliwa sasa

Mika 2: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia