Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Yobu 17

17
1“Nimevunjika moyo, siku zangu zimekwisha,
kaburi langu liko tayari.
2Kweli wanaonidhihaki wamenizunguka,
dhihaka zao naziona dhahiri.
3“Ee Mungu, uwe mdhamini wangu mbele yako,
maana hakuna mwingine wa kunidhamini.
4Maadamu umezifumba akili za rafiki zangu;
usiwaache basi wanishinde.
5Mtu anayewasaliti rafiki zake kwa faida
watoto wake watakufa macho.
6“Nimefanywa kuwa kichekesho kwa watu
nimekuwa mtu wa kutemewa mate.
7Macho yangu yamefifia kwa uchungu;
viungo vyangu vyote vimekuwa kama kivuli.
8Wanyofu wanaduwaa waonapo balaa langu,
nao wasio na hatia hujichochea
dhidi ya mtu wanayedhani hamchi Mungu.
9Hata hivyo, mnyofu hushikilia msimamo wake,
mtu atendaye mema huzidi kuwa na nguvu zaidi.
10Lakini nyinyi njoni, njoni nyote tena,
kwenu sitampata mwenye hekima hata mmoja.
11“Siku zangu zimekwisha, mipango yangu imevunjwa;
matazamio ya moyo wangu yametoweka.
12Kwa hao rafiki zangu usiku ni mchana;#17:12 kilicho … mchana: Au lakini kwenu usiku ni mchana.
je, ndio kusema mna mwanga gizani humu?
13Kwa vile Kuzimu ndio nyumba yangu,
na makao yangu yamo humo gizani;
14kama naliita kaburi ‘baba yangu’
na buu, ‘mama yangu’ au ‘dada yangu’,
15je, nimebakiwa na tumaini gani?
Ni nani awezaye kuona tumaini hilo?
16Tazamio langu litashuka nami kuzimu!
Tutateremka sote wawili hadi huko mavumbini!”

Iliyochaguliwa sasa

Yobu 17: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha