Mwanzo 31:44-49
Mwanzo 31:44-49 BHN
Basi, tufanye agano mimi nawe, liwe ushahidi kati yako nami.” Basi, Yakobo akachukua jiwe, akalisimika kama nguzo ya ukumbusho. Tena Yakobo akawaambia ndugu zake, “Kusanyeni mawe.” Nao wakakusanya mawe na kufanya rundo. Kisha wakala chakula karibu na rundo hilo la mawe. Labani akaliita rundo hilo Yegar-sahadutha, lakini Yakobo akaliita Galeedi. Labani akasema, “Rundo hili ni ushahidi kati yako na mimi leo.” Kwa hiyo Labani akaliita Galeedi, na ile nguzo akaiita Mizpa akisema, “Mwenyezi-Mungu na atulinde tuwapo mbali bila kuonana.