Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Ezekieli 30

30
Mwenyezi-Mungu ataiadhibu Misri
1Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 2“Wewe mtu! Toa unabii useme kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Ombolezeni na kusema: ‘Ole wetu siku ile!’
3Kwa maana, siku hiyo imekaribia;
siku ile ya Mwenyezi-Mungu iko karibu.
Hiyo itakuwa siku ya mawingu,
siku ya maangamizi kwa mataifa.
4Vita vitazuka dhidi ya Misri,
na wasiwasi mkuu utaikumba nchi ya Kushi,
wakati Wamisri wengi wataanguka wameuawa,
mali zao zitakapochukuliwa,
na misingi ya miji yao kubomolewa.
5“Watu wote waliofungamana na Wamisri, yaani watu wa Kushi, Puti, Ludi, Arabia yote na Libia wataangamia pamoja nao.
6“Mimi Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Wote wanaoiunga mkono Misri wataangamia,
mashujaa wake wenye fahari wataangamizwa,
tangu Migdoli mpaka Syene watu watauawa vitani.
Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema.
7Misri itakuwa jangwa kama nchi zilizo jangwa
na miji yake itakuwa magofu kama miji iliyoteketezwa.
8Nitakapoiteketeza Misri kwa moto
na kuwavunjilia mbali wasaidizi wake wote
ndipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.
9Siku hiyo, nitapeleka wajumbe kwenda kuwatisha
Waethiopia wanaojidhani kuwa salama.
Watatetemeka siku Misri itakapoangamia.
Naam! Kweli siku hiyo yaja!
10“Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Nitamtumia Nebukadneza, mfalme wa Babuloni,
kukomesha utajiri wa nchi ya Misri.
11Nebukadneza mwenyewe pamoja na watu wake,
taifa katili kuliko mataifa yote,
watatumwa kuiangamiza nchi ya Misri.
Watachomoa panga zao dhidi ya Misri
na kuijaza nchi hiyo watu waliouawa.
12Nitaukausha mto Nili na vijito vyake,
na kuwauzia watu waovu nchi ya Misri.
Nitasababisha uharibifu nchini kote
kwa mkono wa watu wageni.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
13“Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:
Nitaharibu vinyago vya miungu,
na kukomesha sanamu mjini Memfisi.
Hakutakuwa na mkuu tena huko Misri.
Nitasababisha hofu itawale nchini Misri.
14Mji wa Pathrosi nitaufanya kuwa mtupu,
mji wa Soani nitauwasha moto,
mji wa Thebesi nitauadhibu.
15Nitamwaga ghadhabu yangu juu ya Pelusiumu,
ile ngome inayotegemewa na Misri;
na kuangamiza makundi ya Thebesi.
16Nitaiwasha moto nchi ya Misri.
Pelusiumu utashikwa na dhiki kubwa,
ukuta wa Thebesi utabomolewa,#30:16 ukuta … utabomolewa: Makala ya Kiebrania si dhahiri.
nao Memfisi utakabiliwa na adui mchana wazi.
17Vijana wanaume wa Oni na Pi-besethi watauawa kwa upanga,
na wakazi wengine watachukuliwa uhamishoni.
18Huko Tahpanesi mchana utakuwa giza
wakati nitavunja mamlaka ya Misri
na kiburi chake kikuu kukomeshwa.
Wingu litaifunika nchi ya Misri
na watu wake watachukuliwa mateka.
19Ndivyo nitakavyoiadhibu Misri.
Na watu watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”
Kuvunjwa kwa nguvu za Misri
20Siku ya saba ya mwezi wa kwanza, mwaka wa kumi na moja tangu uhamisho wetu, neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia: 21“Wewe mtu! Nimeuvunja mkono wa Farao mfalme wa Misri, nao haukufungwa ili uweze kupona na kuweza kushika upanga. 22Kwa hiyo, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitapambana na Farao mfalme wa Misri. Nitaivunja mikono yake yote miwili, ule mzima na hata uliovunjika. Na upanga ulio mkononi mwake utaanguka chini. 23Nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa na kuwasambaza katika nchi nyingine. 24Mikono ya mfalme wa Babuloni nitaitia nguvu na kutia upanga wangu mkononi mwake. Lakini nitaivunja mikono ya Farao, naye atapiga kite mbele ya mfalme wa Babuloni kama mtu aliyejeruhiwa vibaya sana. 25Mikono ya mfalme wa Babuloni nitaiimarisha, lakini mikono ya Farao italegea. Hapo watu watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu. Nitakapotia upanga wangu mkononi mwa mfalme wa Babuloni, ataunyosha dhidi ya nchi ya Misri, 26nami nitawatawanya Wamisri kati ya mataifa mengine na kuwasambaza katika nchi nyingine. Ndipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”

Iliyochaguliwa sasa

Ezekieli 30: BHN

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha