Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Matendo 8:14-17

Matendo 8:14-17 BHN

Wale mitume waliokuwa kule Yerusalemu walipopata habari kwamba wenyeji wa Samaria nao wamelipokea neno la Mungu, waliwatuma huko Petro na Yohane. Walipofika waliwaombea hao waumini ili wampokee Roho Mtakatifu; maana wakati huo Roho Mtakatifu hakuwa amemshukia yeyote kati yao; walikuwa wamebatizwa tu kwa jina la Bwana Yesu. Basi, Petro na Yohane wakawawekea mikono hao waumini, nao wakampokea Roho Mtakatifu.