Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zekaria 9

9
Hukumu kwa adui za Israeli
Uaguzi
1 # Zab 145:15; Isa 17:1-3; Yer 49:23-27; Amo 1:3-5 Ufunuo wa neno la BWANA, lililosemwa juu ya nchi ya Hadraki, na Dameski itakuwa mahali pake pa kustarehe; kwa maana jicho la mwanadamu na la kabila zote za Israeli linamwelekea BWANA;#Isa 23:1-18; Eze 26:1—28:26; Yoe 3:4-8; Amo 1:9-10; Mt 11:21-22; Lk 10:13-14 2#Yer 49:23; Amo 1:9; Oba 1:20; Eze 28:3 na Hamathi pia iliyo mpakani mwake; na Tiro, na Sidoni, kwa maana ana akili nyingi. 3Na Tiro alijijengea ngome, akakusanya fedha kama mchanga, dhahabu safi kama matope ya njia kuu. 4#Eze 26:17 Tazama, Bwana atamwondolea mali zake, naye ataupiga uwezo wake alio nao baharini, naye mwenyewe atateketezwa kwa moto. 5#Isa 14:29-31; Yer 47:1-7; Eze 25:15-17; Yoe 3:4-8; Amo 1:6-8; Sef 2:4-7; Mdo 8:26 Ashkeloni ataona haya na kuogopa; Gaza pia, naye atafadhaika sana; na Ekroni, kwa maana matarajio yake yatatahayarika; na mfalme ataangamia toka Gaza, na Ashkeloni atakuwa hana watu. 6Na mwana wa haramu atatawala huko Ashdodi, nami nitakatilia mbali kiburi cha Wafilisti. 7Nami nitaondoa damu yake kinywani mwake, na machukizo yake nitayatoa katika meno yake; yeye naye atakuwa ni mabaki kwa Mungu wetu; naye atakuwa kama mtu mkuu katika Yuda, na Ekroni kama Myebusi. 8#Kum 33:27; Zab 34:7; Kut 3:7 Nami nitapiga kambi yangu pande zote za nyumba yangu ili kuwapinga adui, mtu awaye yote asipite ndani yake wala kurudi; wala mtu aoneaye hatapita tena kati yao; kwa maana sasa nimeona kwa macho yangu.
Mtawala ajaye wa watu wa Mungu
9 # Mt 21:5; Yn 12:15; Zab 2:6; Yn 1:49; Lk 19:38; Isa 45:21; Mdo 22:14; 1 Pet 3:18 Furahi sana, Ee binti Sayuni;
Piga kelele, Ee binti Yerusalemu;
Tazama, mfalme wako anakuja kwako;
Ni mwenye haki, naye ana wokovu;
Ni mnyenyekevu, amepanda punda,
Naam, mwanapunda, mtoto wa punda.
10 # Zab 72:3,8; Isa 11:10; Efe 2:14; Kol 1:20,21; Zab 72:8; Isa 9:6,7; Mik 5:4; Ufu 11:15 Na gari la vita nitaliondoa liwe mbali na Efraimu, na farasi awe mbali na Yerusalemu, na upinde wa vita utaondolewa mbali; naye atawahubiria mataifa yote habari za amani; na mamlaka yake yatakuwa toka bahari hata bahari, na toka Mto hata miisho ya dunia. 11#Isa 61:1; Kut 24:8 Na kwa habari zako wewe, kwa sababu ya damu ya agano lako, nimewatoa wafungwa wako katika shimo lile lisilo na maji. 12Rudini katika ngome yenu, enyi wafungwa wa tumaini; hata hivi leo nasema ya kwamba nitakurudishia maradufu. 13Maana nimejipindia Yuda, nimeujaza upinde wangu Efraimu; nami nitawachochea wana wako, Ee Sayuni, wapigane na wana wako, Ee Ugiriki, nami nitakufanya wewe kuwa kama upanga wa shujaa.
14Naye BWANA ataonekana juu yao,
Na mshale wake utatoka kama umeme;
Na Bwana MUNGU ataipiga tarumbeta,
Naye atakwenda kwa pepo za kisulisuli za kusini.
15 # Law 4:25 BWANA wa majeshi atawalinda;
Nao watakula na kuyakanyaga mawe ya teo;
Nao watakunywa na kufanya kelele kama kwa divai;
Nao watajazwa kama mabakuli, kama pembe za madhabahu.
16 # Eze 37:23; Mal 3:17; Isa 11:12 Na BWANA, Mungu wao, atawaokoa siku hiyo,
Kama kundi la watu wake;
Kwa maana watakuwa kama vito vya taji,
Vikimetameta juu ya nchi yake.
17Maana wema wake, jinsi ulivyo mwingi!
Na uzuri wake, jinsi ulivyo mwingi!
Nafaka itawasitawisha vijana wanaume,
Na divai mpya vijana wanawake.

Iliyochaguliwa sasa

Zekaria 9: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia