Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 85

85
Sala ya kupata fadhili za Mungu tena
Kwa mwimbishaji. Ya Wakorahi. Zaburi.
1 # Yer 30:18; Eze 39:25 BWANA, umeiridhia nchi yako,
Umewarejesha mateka wa Yakobo.
2Umeusamehe uovu wa watu wako,
Umezisitiri hatia zao zote.
3Umeiondoa ghadhabu yako yote,
Umerudi na kuuacha ukali wa hasira yako.
4Mungu wa wokovu wetu, uturudishe,
Uikomeshe hasira uliyo nayo juu yetu.
5Je! Utatufanyia hasira hata milele?
Utadumisha ghadhabu kizazi hadi kizazi?
6 # Hab 3:2 Je! Hutaki kurudi na kutuhuisha,
Ili watu wako wakufurahie?
7Ee BWANA, utuoneshe rehema zako,
Utupe wokovu wako.
8 # Hab 2:1; Zek 9:10; 2 Pet 2:20 Na nisikie atakavyosema Mungu BWANA,
Maana atawaambia watu wake amani,
Naam, na watauwa wake pia,
Bali wasiurudie upumbavu tena.
9Hakika wokovu wake uko karibu na wamchao,
Ndipo utukufu wake ukae katika nchi yetu.
10 # Mik 7:20; Yn 1:17; Zab 72:2,3; Isa 32:17; Lk 2:14; Yn 14:27 Fadhili na kweli zitakutana,
Haki na amani zitakumbatiana.
11 # Isa 45:8; 2 Kor 5:14-21 Kweli itachipuka katika nchi,
Haki itachungulia kutoka mbinguni.
12 # Yak 1:17 Naam, BWANA atatoa kilicho chema,
Na nchi yetu itatoa mazao yake.
13Haki itakwenda mbele zake,
Na kuzitayarishia hatua zake mapito.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 85: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia