Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 70

70
Sala ya ukombozi kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji. Ya Daudi, kama matoleo ya ukumbusho.
1Ee Mungu, uniokoe,
Ee BWANA, unisaidie hima.
2 # Zab 109:29 Waaibike, wafedheheke,
Wanaoitafuta nafsi yangu.
Warudishwe nyuma, watahayarishwe,
Wapendezwao na shari yangu.
3Warudi nyuma, na iwe aibu yao,
Wanaosema, Ewe! Ewe!
4 # Isa 61:10; Hab 3:17; Rum 5:2; Flp 3:1; 1 Pet 1:2-9 Washangilie, wakufurahie,
Wote wakutafutao.
Waupendao wokovu wako
Waseme daima, Atukuzwe Mungu.
5 # Zab 40:17; Amu 5:28; Zab 141:1; Ebr 10:37; Ufu 22:20 Nami ni maskini na mhitaji,
Ee Mungu, unijilie kwa haraka.
Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu,
Ee BWANA, usikawie.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 70: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia