Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 7

7
Ombi la msaada juu ya watesaji
Ombolezo la Daudi, aliloimba kwa BWANA kuhusu Kushi, Mbenyamini.
1BWANA, Mungu wangu, nimekukimbilia Wewe,
Uniokoe na wote wanaonifuatia, uniponye.
2 # 1 Pet 5:8 Asije akaipapura nafsi yangu kama simba,
Akaniburura hadi pasipokuwa na wa kuniponya.
3 # 2 Sam 16:7 BWANA, Mungu wangu, ikiwa nimetenda haya,
Ikiwa mna uovu mikononi mwangu,
4 # 1 Sam 24:7 Ikiwa nimemlipa mabaya
Yeye aliyekaa kwangu salama;
(Hasha! Nimemponya yeye
Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)
5Basi adui na anifuatie,
Na kuikamata nafsi yangu;
Naam, aukanyage uzima wangu,
Na kuulaza utukufu wangu mavumbini.
6 # Zab 94:2 BWANA uondoke kwa hasira yako;
Ujiinue Juu ya ujeuri wa watesi wangu;
Uamke kwa ajili yangu;
Umeamuru hukumu.
7Kusanyiko la mataifa na likuzunguke,
Na juu yake uketi utawale.
8BWANA atawaamua mataifa,
BWANA, unihukumu mimi,
Kwa kadiri ya haki yangu,
Kulingana na unyofu nilio nao.
9 # Ufu 2:23; 1 Sam 16:7 Ubaya wao wasio haki na ukome,
Lakini umthibitishe mwenye haki.
Kwa maana mjaribu mioyo na fikira
Ndiye Mungu aliye mwenye haki.
10Ngao yangu ina Mungu,
Awaokoaye wanyofu wa moyo.
11Mungu ni mwamuzi mwenye haki,
Naam, Mungu akasirikiaye waovu kila siku.
12Mtu asipoongoka ataunoa upanga wake;
Ameupinda uta wake na kuuweka tayari;
13Naye amemtengenezea silaha za kuua,
Akifanya mishale yake kuwa mipini ya moto.
14Tazama, huyu ametunga uovu,
Amechukua mimba ya madhara, amezaa uongo.
15 # Est 7:10; Mit 5:22 Amechimba shimo, amelichimba chini sana,
Akatumbukia katika handaki aliyoichimba!
16 # 1 Fal 2:32 Madhara yake yatamrejea kichwani pake,
Na dhuluma yake itamshukia utosini.
17Nitamshukuru BWANA kwa kadiri ya haki yake;
Nitaliimbia jina la BWANA aliye juu.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 7: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia