Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 31

31
Sala na sifa kwa kukombolewa kutoka kwa adui
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1Nimekukimbilia Wewe, BWANA,
Nisiaibike milele.
Kwa haki yako uniponye,
2 # Zab 71:2; Mit 22:17 Unitegee sikio lako, uniokoe hima.
Uwe kwangu mwamba wa nguvu,
Ngome thabiti ya kuniokoa.
3 # Zab 23:3; Yer 14:7 Ndiwe mwamba wangu na ngome yangu;
Kwa ajili ya jina lako uniongoze na unichunge.
4Utanitoa katika wavu walionitegea kwa siri,
Maana Wewe ndiwe ngome yangu.
5 # Lk 23:46; Mdo 7:59; 2 Tim 1:12; Ebr 6:18 Mikononi mwako naiweka roho yangu;
Umenikomboa, Ee BWANA, Mungu wa kweli.
6Nawachukia wao washikao yasiyofaa yenye uongo;
Bali mimi namtumainia BWANA.
7 # Yn 10:27 Na nishangilie, nizifurahie fadhili zako,
Kwa kuwa umeyaona mateso yangu.
Umeijua nafsi yangu taabuni,
8 # Zab 18:19 Wala hukunitia mikononi mwa adui;
Miguu yangu umeisimamisha mahali penye usalama.
9Ee BWANA, unifadhili, maana ni katika dhiki,
Jicho langu limenyauka kwa masumbufu,
Naam, mwili wangu na nafsi yangu.
10Maana maisha yangu yamekwisha kwa huzuni,
Na miaka yangu kwa maumivu.
Nguvu zangu zimeniishia kwa uovu wangu,
Na mifupa yangu imepooza.
11 # Zab 88:8 Kwa sababu ya watesi wangu nimelaumiwa,
Naam, hasa kwa jirani zangu;
Na kitu cha kutisha kwa rafiki zangu;
Wanaoniona njiani wananikimbia.
12Nimesahauliwa kama mfu asiyekumbukwa;
Nimekuwa kama chombo kilichovunjika.
13 # Yer 20:3; Omb 2:22; Mt 27:1 Maana nimesikia wengi wakinong'onezana;
Hofu katika pande zote.
Waliposhauriana juu yangu,
Walipanga kunitoa uhai wangu.
14Lakini mimi nakutumaini Wewe, BWANA,
Nimesema, Wewe ndiwe Mungu wangu.
15Nyakati zangu zimo mikononi mwako;
Uniponye kutoka kwa adui zangu na wanaonifuatia.
16 # Hes 6:25; Zab 4:6; Dan 9:17 Umwangaze mtumishi wako
Kwa nuru ya uso wako;
Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.
17 # Zab 25:2 Ee BWANA, nisiaibishwe, maana nimekuita;
Waaibishwe wasio haki, wanyamaze kuzimuni.
18 # Zab 12:3 Midomo ya uongo iwe na ububu,
Imneneayo mwenye haki maneno ya kiburi,
Kwa majivuno na dharau.
19 # Isa 64:4; 1 Kor 2:9 Jinsi zilivyo nyingi fadhili zako
Ulizowawekea wakuchao;
Ulizowatendea wakukimbiliao
Mbele ya wanadamu!
20 # Zab 27:5; Ayu 5:21 Utawasitiri kutoka kwa fitina za watu
Katika maficho ya kuwapo kwako;
Utawaficha katika hema
Na ushindani wa ndimi.
21BWANA ahimidiwe; kwa maana amenitendea
Fadhili za ajabu nilipozongwa kama mji wenye boma.
22Nami nilisema kwa pupa yangu,
Nimekatiliwa mbali na macho yako;
Lakini ulisikia sauti ya kilio changu
Wakati nilipokulilia.
23 # 1 Pet 1:5 Mpendeni BWANA,
Ninyi nyote mlio watauwa wake.
BWANA huwahifadhi waaminifu,
Bali humlipiza mwenye kiburi ipasavyo.
24Iweni hodari, na mpige moyo konde,
Ninyi nyote mnaomngoja BWANA.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 31: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha