Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 20

20
Sala ya ushindi
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 # Isa 50:10 BWANA akujibu siku ya dhiki,
Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.
2Akutumie msaada toka patakatifu pake,
Na kukutegemeza toka Sayuni.
3Azikumbuke sadaka zako zote,
Na kuzitakabali dhabihu zako.
4 # 1 Yoh 5:14,15 Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako,
Na kukutimizia mipango yako yote.
5 # Isa 12:1,2; 1 Sam 17:45 Na tuushangilie wokovu wako,
Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu.
BWANA akutimizie matakwa yako yote.
6Sasa najua kuwa BWANA amwokoa masihi#20:6 Au, mtiwa mafuta. wake;
Atamjibu toka mbingu zake takatifu,
Kwa matendo makuu ya wokovu
Ya mkono wake wa kulia.
7 # Amu 7:7 Hawa wanataja magari na hawa farasi,
Lakini sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.
8Wao wameinama na kuanguka,
Bali sisi tumeinuka na kusimama.
9BWANA, umwokoe mfalme,
Utuitikie siku tuitayo.

Iliyochaguliwa sasa

Zaburi 20: SRUV

Kuonyesha

Shirikisha

Nakili

None

Je, ungependa vivutio vyako vihifadhiwe kwenye vifaa vyako vyote? Jisajili au ingia

YouVersion hutumia vidakuzi kubinafsisha matumizi yako. Kwa kutumia tovuti yetu, unakubali matumizi yetu ya vidakuzi kama ilivyoelezwa katika Sera yetu ya Faragha