Chapa ya Youversion
Ikoni ya Utafutaji

Zaburi 122:1-9

Zaburi 122:1-9 SRUV

Nilifurahi waliponiambia, Twende nyumbani kwa BWANA. Miguu yetu imesimama Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu. Ee Yerusalemu uliyejengwa Kama mji ulioshikamana, Huko ndiko wapandako kabila, makabila ya BWANA; Kama ulivyowaamuru Waisraeli, Walishukuru jina la BWANA. Maana huko viliwekwa viti vya hukumu, Viti vya enzi vya ukoo wa Daudi. Uombeeni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao; Amani na ikae ndani ya kuta zako, Na kufanikiwa ndani ya majumba yako. Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe. Kwa ajili ya nyumba ya BWANA, Mungu wetu, Nitakuombea mema.

Soma Zaburi 122

Mipango ya Kusoma Bila Malipo na Ibada zinazohusiana na Zaburi 122:1-9